McEddy Elroy

Thursday, October 28, 2010

UPASUAJI WAOKOA MACHO YA WATU 33 IRINGA

Mratibu wa huduma za Afya ya macho na Daktari wa macho mkoani Iringa akimpima macho mgonjwa wa macho.Picha nyingine ni muuguzi akimfunga dawa mgonjwa aliyefanyiwa upasuaji na wengine ni wagonjwa waliofanyiwa upasuaji wa macho katika kituo cha Afya Malangali wilayani Mufindi hivi karibuni.

Tuesday, October 5, 2010

TUNADI SERA ZETU

Wagombea ubunge katika jimbo la Kalenga Mkoani Iringa kutoka kushoto na vyama vyao kwenye mabano ni John Katindasa (TLP), Rehema Makoga (Chadema) na Ismail Makuke (Jahazi Asilia) wakijibu maswali ya wapiga kura katika mdahalo wa wagombea na wapiga kura wa jimbo hilo uliofanyika kwenye ukumbi wa serikali ya kijiji.Mgombea wa CCM,Dk.William Mgimwa hakuwepo kwenye mdahalo kutokana marufuku ya CCM kwa wagombea wa ngazi zote kuhudhuria midahalo.

MGOMBEA WA UBUNGE KALENGA KUPITIA TLP AKIWA HANA LA KUFANYA

Mgombea wa Ubunge Jimbo la Kalenga,kupitia Chama cha TLP,John Katindasa (Mwenye suti nyeusi katikati) akiwa hana la kufanya baada ya gari lake kugoma kuwaka muda mfupi baada ya kumalizika kwa mdahalo wa wagombea na wapiga kura wa Jimbo la Kalenga.Wengine walioshiriki mdahalo huo ni Mgombea wa kupitia Chadema, Rehema Makoga na mgombea kutia Jahazi Asilia,Ismail Makuke.