McEddy Elroy

Sunday, December 26, 2010

WAFANYAKAZI WA TANESCO IRINGA WATOA ZAWADI YA X-MASS KWA YATIMA TOSAMAGANGA

Meneja wa Tanesco Mkoa wa Iringa Mhandisi John Bandiye akikabidhi zawadi mbalimbali kwa Mkuu wa kituo cha yatima Tosamaganga,Sista Hellena Kihwele.

Wafanyakazi wa Tanesco Mkoa wa Iringa walijichangisha kutoka mifukoni mwao na kwenda kuwapa zawadi watoto hao kama ishara ya upendo na kuwajali. Zawadi zilizotolewa ni mchele kilo 100,sukari kilo 50,mayai trei tatu, chunzi katoni moja na sabuni ya kufulia katoni tano, vyote vikiwa na thamani ya zaidi ya Sh.500,000/-.

No comments:

Post a Comment