McEddy Elroy

Saturday, February 5, 2011

DR.Kiiza Besigye aikosoa Serikali ya Uganda

Kiongozi wa upinzani nchini Uganda na mgombea kiti cha Urais Kanali Mstaafu Dr Kiiza Besigye ameikosoa serikali ya sasa ya National Resistance Movement –NRM, kwa kupuuza malengo yaliyosababisha vita vya msituni ambavyo hatimae vilisababisha kundi la uasi a NRM kutwaa madaraka miaka 30 iliopita.

Ameyasema katika mkutano na waandishi habari mjini Kampala, akitoa ujumbe kwa jeshi hilo wakati likijiandaa kusherehekea miaka 30 ya kuasisiwa. Sherehe hizo zitafanyika mwishoni mwa juma.

Kiiza Besigye ambae zamani alikuwa katika jeshi la taifa na sasa ni mkosoaji kuu wa serikali hiyo, ameishutumu serikali ya NRM kwa kupoteza lengo la kile walichopigania wakati walipoanzisha mapambano miaka 30 iliopita.

Besigye alikuwa anagusia siku ya tarehe sita ambayo itasherehekewa Jumapili.

Katika hali inayosemekana kama kutumiwa jeshi kumpendelea mpinzani wake wa chama tawala cha NRM, Rais Yoweri Museveni, Besigye ameonya wanajeshi kujizuia kutumiwa na watu ambao wanataka kuwakatisha tamaa wananchi wa Uganda.

Nalo Jeshi kwa upande wake limesema limefanya mengi tangu wakati huo kama vile uhuru wa kusema na mengine mengi.

No comments:

Post a Comment