McEddy Elroy

Sunday, December 26, 2010

WAFANYAKAZI WA TANESCO IRINGA WATOA ZAWADI YA X-MASS KWA YATIMA TOSAMAGANGA

Meneja wa Tanesco Mkoa wa Iringa Mhandisi John Bandiye akikabidhi zawadi mbalimbali kwa Mkuu wa kituo cha yatima Tosamaganga,Sista Hellena Kihwele.

Wafanyakazi wa Tanesco Mkoa wa Iringa walijichangisha kutoka mifukoni mwao na kwenda kuwapa zawadi watoto hao kama ishara ya upendo na kuwajali. Zawadi zilizotolewa ni mchele kilo 100,sukari kilo 50,mayai trei tatu, chunzi katoni moja na sabuni ya kufulia katoni tano, vyote vikiwa na thamani ya zaidi ya Sh.500,000/-.

Tuesday, December 7, 2010

MAWAZO YA MLIPUAJI WA KUJITOA MHANGA

Mambomu ya kujitoa mhanga yamekuwa mtindo wa mashambulio ya kisiasa katika zama zetu hizi. Kuanzia Afghanistan hadi Madrid, London mpaka Sri Lanka, mabomu hayo yamekuwa katika maisha ya kila siku ya kisiasa na ni mbinu muhimu inayotumiwa katika ugaidi wa kisasa.

Wakati uchunguzi wa milipuko ya Julai 7 jijini London ukiendelea kufanyika na kujaribu kuona kipi kilijiri siku hiyo, utafiti mdogo sana umefanyika kutazama nini hasa wanawaza walipuaji wenyewe wa kujitoa mhanga.

Sababu

Kujaribu kugundua hasa kwa nini mlipuaji wa kujitoa mhanga, anajiua ili kuendeleza harakati fulani, ni vigumu mno, na ni kwa sababu ambazo zinazoeleweka kabisa.

Lakini utafiti mmoja uliofanywa na Chuo Kikuu cha Tel Aviv, nchini Israel, umefanya bidii kujaribu kugundua iwapo walipuaji wa kujitoa mhanga wana tabia zozote zinazoonekana. Wamefanya hivyo kwa kuzungumza na kufanya tathmini ya watu waliokuwa wawe walipuaji wa kujitoa mhanga.

Watu hao, ambao walijaribu kufanya mashambulio ya kujitoa mhanga, lakini walishindwa kwa sababu mbalimbali, ikiwemo matatizo ya kiufundo (bomu halikulipuka) au kukamatwa kabla ya kujilipua (wakielekea kujilipua au mapema kabla ya hapo).

Msongo wa mawazo

Watafiti waligundua mkondo wa watu ambao hawana uwezo mkubwa wa kuhimili wanapojikuta katika hali ya msongo, au mfadhaiko utokanao na shida (stress). Aidha pia waligundua kuwa watu hao hawana uwezo wa 'kuona mbali' na pia kuwa na tabia ya kutishwa na watu wenye madaraka.

Vilevile wamegundua kuwa, watu wanaowaandaa walipuaji wa kujitoa mhanga, wana ubinafsi mkubwa, wana uwezo mkubwa wa kiakili kupambana na msongo, na mara nyingi, wenyewe hawako tayari kuwa walipuaji wa kujitoa mhanga.

Profesa mstaafu, na mtaalam wa masuala ya ugaidi Ariel Merari, aliweza kukutana na watu 15 waliokuwa wakitaka kujilipua, ambao wako gerezani, kwa tuhuma za mashambulio yanayohusiana na mzozo wa Israel na Palestina.

Watano kati yao, walikuwa wametumwa na kundi la Hamas, watano na kundi la Islamic Jihad na watano kutoka kundi la al-Aqsa la Fatah.

Waandaaji

Aidha, Profesa Merari na wataalam wenzake waliziungumza na waandaaji wa walipuaji hao, wote kutoka makundi hayo.

Mbali na waandaaji hao na walipuaji wa kujitoa mhanga, kulikuwa na kundi la udhibiti. Kundi hilo la watu 12 walikuwa wameshitakiwa na kufungwa kwa ghasia mbalimbali za kisiasa kuanzia urushaji mawe hadi mashambulizi ya kutumia silaha.

Changamoto ya kwanza kwa kikosi cha Profesa Merari ilikuwa kuwashawishi watu hao kuzungumza. Wafungwa hao walisisitiza kupata ruhusa kwanza kutoka kwa wakubwa wa makundi yao.

"Niliwaambia sababu za sisi kufanya utafiti huu," amesema Profesa Merari akizungumza na kituo cha BBC Radio 4.

"Kulikuwa na mjadala mzito. Mwishowe walikubali kushiriki na hakika hiyo ndio ilikuwa hatua muhimu kupata wengine kuweza kuzungumza."

Katika miaka ya hivi karibuni, ulipuaji wa kujitoa mhanga umeongezeka duniani.Kati ya mwaka 1981 na 2000, nchi 17 zimeathiriwa na mashambulio ya kujitoa mhanga, ikilinganishwa na nchi 32 kati ya mwaka 2001 na 2008.

Waumini

Mashambulio ya kujitoa mhanga mara nyingi huhusishwa na mtazamo wa itikadi kali za kidini kutoka kwa mshambuliaji.

Hata hivyo, utafiti huu mpya unasema, umuhimu wa dini haukupewa nafasi ya juu, ikilinganishwa na sababu nyingine, wakati wafungwa hao wakizungumzia wakati wakifanya uamuzi wa kuendesha mashambulio hayo ya kujilipua.

"Karibu wote walikuwa watu wanaofuata dini, lakini waliokuwa wakitaka kujilipua hawakuwa waumini sana kama wale wanaowadhibiti.

"Undani na ukubwa wa imani ya kidini haukuwa jambo ambalo liliwatofautisha kati yao na magaidi wasiotumia njia ya kujilipua."

Badala yake, Profesa Merari amegundua kuwa "Kuaibishwa kwa taifa" ndio sababu kuu ya kufanya mashambulio hayo.

"Hii ndio sababu kubwa, ya wazi na yenye nguvu iliyowapa ari ya kufanya hivyo.

"Sio suala la mtu kuteseka binafsi; walijaribu kulipiza kisasi kwa niaba ya jamii yao inayoteseka. wametaja matukio ambayo wameyaona katika televisheni, na sio matukio yaliyowatokea wao binafsi."

Watu waliohojiwa katika nafasi ya uandaaji wa walipuaji, walikuwa kwa wastani wakubwa kiumri, wenye elimu ya kutosha na ambao wasingependa wao kujitokeza na kujilipua.

Tisa kati ya 14 walikiri kuwa wasingekuwa tayari wao wenyewe kujilipua, kwa sababu- walikuwa wanaogopa kufanya hivyo

"Hawakutumia neno 'kuogopa', lakini walitumia maneno kama vile 'sio kila mtu anaweza kufanya hivyo', au 'inahitaji mtu mwenye hiba ya kipekee' na maneno kama hayo.

"watano waliosalia walisema 'kimsingi ningependa kufanya hivyo, lakini kazi yangu kama kamanda ni muhimu kwa hiyo sikuweza kufanya hivyo'. Walikuwa waoga tu nadhani, katika kutoa jibu la moja kwa moja."

Picha halisi

Utafiti huo pia uligundua kuwa taswira inayowekwa na waandaaji wa walipuaji wa kujitoa mhanga, kuwa "ni vijana wenye dhamira kubwa" ni jambo la kupotosha.

"Walipuaji wa kujitoa mhanga wenywe wametoa taswira tofauti kabisa. Asilimia sitini na sita walikiri kuwa walikuwa wakiogopa kufanya hivyo, au walikuwa wakisita. Na tulivyochunguza idadi kubwa ya matukio ya kujilipua, tuligundua asilimia 36 ya matukio 61 ya walipuaji wa kujitoa mhanga, waliamua kuacha kufanya hivyo.

Profesa Merari anakiri kuwa, kwa sababu watu wote waliozungumza nao wametokana na majaribio "yaliyoshindwa kufanikiwa", utafiti huu hauwezi kutoa picha halisi ya mlipuaji wa kujitoa mhanga.

Hata hivyo, timu hiyo ya wataalamu inaamini utafiti huo unatoa "picha ya karibu zaidi".

"Baadhi ya walipuaji hawa wa kujitoa mhanga walifika kabisa na katika maeneo waliyotakiwa kujilipua, na hata kubonyeza kitufe cha kujilipua, lakini mabomu waliyokuwa wameyabeba hayakulipuka, kutokana na sababu za kiufundi.

"Kisaikolojia, hawa ni walipuaji wa kujitoa mhanga kwa kila mtazamo."

Utafiti wake huu unafikia majumuisho kuwa, hatua zinaweza kuchukuliwa kuzuia mashambulizi kwa misingi ya kutazama haiba na tabia ya mtu.

"Moja ya majumuisho ya utafiti huu ni kuwa kizuizi chochote kitakapomkabili mlipuaji wa kujitoa mhanga, kunaongeza nafasi ya mlipuaji huyo kubadili mawazo yake kutekeleza shambulio. Hii ni kwa sababu, wale wanaosita huhitaji kisingizio cha kutofanya shambulio.

"Wanahitaji kisingizio ili wasipoteze heshima yao binafsi.

"Kikwazo chochote, kitakwimu, kitaongeza nafasi ya mlipuaji wa kujitoa mhanga kubadili mawazo yake, akiwa njiani kwenda kujilipua."

Wednesday, December 1, 2010

HIV is the best thing that happened to our marriage

The news could not have come at a worse time. She was just about to give birth to her third child when she learnt that she was HIV-positive.

To make matters worse, she was in an unhappy marriage, a marriage that was headed for the rocks.

“It was just too much for me to process. I was so stunned, I could not even cry,” says 32-year-old Halima Maina.

That was four years ago. Today, Halima and her 36-year-old husband Maina Muriuki say that being diagnosed with HIV turned out to be the saving grace of their once shaky marriage.

“Our marriage is happier and more fulfilling than it was before we found out that we were HIV-positive. We’re better people,” Halima says.

As Maina revisits his former life, one begins to understand Halima’s strange declaration about their marriage being transformed into a happier union by the HIV virus.

“I do not think I would be alive today, if I was HIV-negative,” Maina begins.

He confesses that before knowing his HIV status, alcohol and friends took priority over everything in his life, including his family.

His relationship with his wife was in such tatters that she had contemplated walking out on their 11-year marriage several times.

“He was my husband but I really did not know him because he was rarely home. When he was there, he was too drunk to make sense,” recalls Halima.

Their two sons knew even less of the perpetual drunkard they called daddy.

Maina concedes that the bond between him and his children was even weaker than that with his wife.

To begin with, his job then — a salesman with a local pharmacist — entailed a lot of travelling. He would come back in the wee hours, more often than not drunk.

The boys counted themselves lucky if they saw their father at least once a week, least of all while sober.

“I would leave the house at five in the morning and return late at night, drunk,” he confesses.

Then in the middle of all this gloom, HIV came knocking.

First, Muriuki fell ill and was admitted to Tumutumu Mission Hospital for eight days. His wife was pregnant then, and set to give birth any time. As he lay in his hospital bed, weak and helpless, she delivered their last child, a boy they named Douglas.

It was just before this delivery that the couple learnt about their HIV status. The news was devastating for both of them, so devastating that after being discharged from hospital, Maina fell ill again and was bedridden for five months.

That left his wife to cope alone, not just to nurse their youngest child, but to face the reality of their HIV status alone. Maina was in denial.

Halima says that she was the first to recover. By the time her husband came round to accepting his status, she had nursed their baby for almost six months and was ready to face life and this potent virus called HIV, to which she had never given a thought before.

And suddenly, their roles changed. The strong-willed husband who rarely spent time with his family unexpectedly found himself seeking the comfort of his soft-spoken wife who had quietly borne his truancy for eight years.

Like many men who are confronted with such unexpected news about their HIV status, Maina feared that his wife would leave him. After all, there was no doubt that he was the one who had infected her.

“I took full responsibility. I knew I was the one who infected her because a woman I had been intimate with had died a couple of years back from what I am now convinced was Aids,” says Maina.

Halima did the unexpected. She stayed and chose to confront the virus — and fight for her marriage. It wasn’t easy, though.

“I cried a lot. I asked where I was headed. Did I want my children to live without a father? Eventually, I decided to stay. I chose to live,” says Halima.

She does not regret her decision. Their marriage, she says, has moved to a higher level, one of love, respect, and friendship. Maina is a changed man. He has kicked a habit he had been struggling with for years: alcoholism. He says he now finds the smell of alcohol revolting.

“My drinking friends saw more of me than my wife. But after I was diagnosed HIV-positive, I began a new life,” he says.

His three sons, now aged 11, eight, and four, see more of their father and enjoy a healthy, and easy-going father-son relationship.

“He spends a lot with them,” says Halima.

For this mother of three, HIV has given her what she had quietly longed for during the many dark nights she spent alone with the children — a husband.

“I spent many lonely nights alone, agonising over what he was up to,” she recalls. “In so many ways, this virus that is so feared has given me back my husband.

If he did not know his status, I doubt I would have a husband today.”

Halima has changed, too. According to her husband, she was a rather submissive housewife who quietly slipped behind the shadows of married life, as if she was trying to be invisible.

Well, not anymore.

Today, this mother-of-three plays a bigger role in all the major decisions that the family makes than she did before.

Often, she strictly enforces all the decisions made in their home, like those regarding the family diet.

She ensures that everyone, especially her husband, eats a balanced meal with the little resources available.

She is also a stronger character.

“Before, I was a quiet housewife waiting for my husband to come home. I rarely questioned his behaviour. Not anymore. I have a voice now, and I know that I am entitled to respect and appreciation from my husband, which I am getting.”

And although her husband is currently jobless and relies on odd jobs to provide for them, Halima says that they are happier.

“The bond between us has strengthened. We spend more time together, we share our thoughts more freely. I can now confidently say that we’re a happily married couple,” agrees Maina.

Initially, they feared that those who knew them would shun them because of their status and kept this information to themselves.

But they decided to shake off this fear and begun telling people about their status.

“If sharing our story could help other couples make decisions that would safeguard their health and marriage, we would share it,” says Maina.

They occasionally volunteer as peer counsellors for local support groups of people living with HIV and Aids, in Karatina, Central Kenya, where they come from.

They also talk to married couples about the importance of HIV testing, and over time, the community around them has embraced them.

In a society where an HIV diagnosis begins a despairing mental journey dogged by stigma for many, Maina and his wife have become an inspiration.

They are a poster couple for HIV/Aids anti-stigma campaigns, whose message is perhaps more powerful than any HIV testing and counselling billboard on the streets.

According to the coordinator of the Karatina Home Based Care and Counselling Centre, Samuel Kimiru, the Mainas form the backbone of a team that is encouraging married couples to know their HIV status.

“Many couples are now attending counselling sessions and those who are not married are now able to bargain for safe sex,” says Kimiru.

The result is yet another victory against the spread of HIV and Aids in marriage.

Saturday, November 27, 2010

CHUO KIKUU KISHIRIKI CHA ELIMU MKWAWA TAABANI

Lango Kuu la kuingilia Chuo Kikuu Mkwawa.
Moja ya jengo lenye vyumba vya madarasa Chuoni Mkwawa. Linaonekana kama jengo la utawala. lahasha.Chuo hicho hivi sasa ndiyo kwanza kimepata fedha za ujenzi wa jengo la utawala, kwa sasa Mkuu wa Chuo na wafanyakazi wote watanatumia vyumba vilivyokuwa vya madarasa ya shule ya sekondari Mkwawa kama ofisi zao na mambo mengine ya utawala.
Baadhi ya mabweni ya wanafunzi Chuo Kikuu Mkwawa
Baadhi ya wahitimu wa shahada katika fani mbalimbali kwenye mahafali ya pili ya Chuo Kikuu kishiriki cha Elimu Mkwawa (Muce)

CHUO KIKUU KISHIRIKI CHA ELIMU MKWAWA TAABANI

CHUO Kikuu kishiriki cha Elimu Mkwawa (MUCE) cha Mkoani Iringa, kina majukumu makubwa ya kitaifa ambayo ni pamoja na kusaidia au kuchangia upanuzi wa elimu nchini.

Chuo hiki kimepewa heshima kubwa na Taifa ya kuhakikisha kuwa kinawaandaa walimu wenye sifa sitahiki kutekeleza yale yanayotarajiwa na Taifa. Kinatakiwa kuwaandaa wanafunzi wake kwa ajili ya ulimwengu ujao wa ajira,ulimwengu wa utandawazi na ushindani mkubwa.

Chuo hiki ni muhimu kwa sababu kinasaidia kuondosha tatizo kubwa na la muda mrefu la upungufu wa walimu wenye shahada linaloikabili Taifa kwa muda mrefu.

Hata hivyo,licha ya majukumu haya mazito ya kitaifa,Chuo Kikuu cha Mkwawa kinakabiliwa na changamoto nyingi kiasi kwamba baadhi ya wanafunzi wa mwanzo kusoma hapo, Chuo hicho kilipoanza rasmi mwaka 2005/2006 walifikia hatua ya kudai kuwa Serikali imewapeleka pale ili kuwatunuku shahada za majaribio kwa madai kuwa walikuwa wanasoma katika mazingira magumu mno yasiyostahili kuitwa Chuo Kikuu.

Kuanzishwa kwa MUCE:

Chuo Kikuu cha Mkwawa kilianzishwa rasmi mwaka 2005 baada ya iliyokuwa shule ya sekondari ya Mkwawa (Mkwawa High School) kuvunjwa na wanafunzi waliokuwa hapo kuhamishiwa katika shule za sekondari za Ifunda na Songea Girls.

Chuo Kikuu kishiriki cha Elimu Mkwawa sambamba na Chuo Kikuu kishiriki cha Elimu Changómbe vilianzishwa ili kukabiliana na tatizo kubwa la uhaba wa walimu wenye shahada wa shule za sekondari nchini baada ya Serikali kufanikiwa sana kupitia Mpango wa Maendeleo ya Elimu ya Msingi (MMEM).

Wanafunzi wengi walikuwa wanakwenda shule za sekondari lakini changamoto kubwa ikawa ni vyumba vya madarasa katika shule za sekondari pamoja na walimu wa shule hizo.

Wakati Serikali ikianzisha Mpango wa Maendeleo ya shule za Sekondari (MMES) ili kukabiliana na tatizo la madarasa na majengo ya sekondari kwa jumla, iliona pia kuna haja ya kwenda sambamba na utatuaji wa tatizo au changamoto ya upungufu wa walimu wenye shahada wa shule za sekondari nchini, ndipo wazo likaja la kufunga shule za sekondari Mkwawa na Chuo cha ufundi Chang´ombe ili maeneo hayo yapandishwe hadhi na kuwa Vyuo vikuu vishiriki vya elimu vya Chuo Kikuu cha Dar-Es-Salaam.

Changamoto zinazoikabili MUCE:

Wakati kinaanza rasmi,mwaka 2006/2007 Chuo Kikuu cha Mkwawa kilidahili wanafunzi 1,176. Licha ya ukarabati mdogo uliokuwa umefanyika, wanafunzi hao pamoja na wahadhiri wa Chuo hicho,kwa sehemu kubwa walilazimika kutumia miundombinu iliyorithiwa kutoka shule ya sekondari ya Mkwawa.

Udahili wa wanafunzi katika Chuo hicho umeendelea kuongezeka mwaka na hata mwaka ambapo mwaka 2007/2008 kilidahili wanafunzi 846, mwaka 2008/2009 wanafunzi 654, mwaka 2009/2010 wanafunzi 822 na mwaka huu, yaani 2010/2011 wamedahiliwa wanafunzi 878.

Licha ya ongezeko hilo la wanafunzi,miuondombinu ya Chuo Kikuu kishiriki cha Elimu Mkwawa imeendelea kuwa haikidhi mahitaji ya wanafunzi na wahadhiri.

Katika hali isiyo ya kawaida, katika mahafali ya pili ya MUCE yaliyoafanyika Novemba 20,mwaka huu, wazungumzaji wote katika sherehe za mahafali hayo walijikita zaidi kulalamikia matatizo au changamoto zinazoikibili Chuo hicho, malalamiko kama hayo, mara nyingi kusema kweli yanasikika zaidi katika shule za sekondari hususan za Kata.

Katika mahafali hayo,wanafunzi 677 kati yao wanawake 181 walitunukiwa shahada katika fani nne ambazo ni shahada ya Elimu ya Jamii na Ualimu (481) shahada ya Elimu katika Sayansi za Jamii (102), shahada ya Sayansi na Ualimu (74) na shahada ya Elimu katika Sayansi (20).

Akizungumza katika mahafali hayo,Mwenyekiti wa Bodi ya Usimamizi ya Chuo Kikuu kishiriki cha Elimu Mkwawa na Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dar-Es-Salaam,Professa Rwekaza Mukandala alisema ni wazi kuwa mafunzo bora yanahitaji uboreshaji miundombinu pamoja na rasilimali nyingine zinazohitajika katika kuwaandaa vyema wanafunzi.

“Chuo kinathamini misaada yote inayoendelea kutolewa na serikali ili kuhakikisha kuwa mazingira ya Chuo ni wezeshaji kwa ufundishaji,utafiti na huduma kwa jamii. Mchango wa serikali utaweza kuhakikisha kuwa mahitaji muhimu kwa mafunzo ikiwa ni pamoja na kumbi za mihadhara,madarasa,maabara,maktaba,zana mbalimbali za masomo na mahitaji mengine vinapatikana,” anasema Professa Mukandala.

Professa Mukandala alisema kuwa wakati Chuo kinatambua mchango mkubwa wa serikali,kwa upande mwingine msaada unaotolewa umekuwa kidogo ikilinganishwa na mahitaji halisi na mipango ya Chuo.

“Kwa mfano,kutokana na uhaba huu, wakati ambabo matarajio ya Chuo yalikuwa ni kudahili wanafunzi 1,000 katika mwaka wa masomo 2009/2010 na wanafunzi 1,300 katika mwaka wa masomo 2010/2011,Chuo kimefanikiwa kudahili wanafunzi 800 na 878 tu katika miaka hiyo ya masomo na hii imetokana na uwezo mdogo wa miundombinu iliyopo Chuoni ikiwa ni pamoja na rasilimali nyingine husianifu za watu,” anaongeza Professa Mukandala.

Naye Mkuu wa Chuo Kikuu kishiriki cha Elimu Mkwawa,Professa Phillemon Mushi anasema kwa upande wa malazi ya wanafunzi,Chuo bado kina nafasi 1,100 tu katika mabweni yaliyopo hivyo wanafunzi 737 sawa na asilimia 40.2 wanakaa nje ya Chuo ambapo hakuna uhakika wa mazingira muafaka ya kuweza kufanya kazi zao kama wale ambao wako ndani ya mabweni ya Chuo.

“Hili ni mojawapo ya mambo yanayoweza kuchangia wanafunzi kutofanya vizuri kama ambavyo wangeweza kama mazingira yangekuwa yanakubalika,” alisema Professa Mushi na kuongeza:

“Inaeleweka kuwa katika nchi nyingi suala la mabweni sio kipaumbele kwa Vyuo, ila hapa Tanznania na hususan hapa Iringa ni kipaumbele kwa sababu nje ya Chuo Kikuu cha Mkwawa hakuna nyumba za kutosha zinazofaa kwa malazi ya wanafunzi, ombi letu ni kwamba serikali ikiwezeshe Chuo au wawekezaji kujenga mabweni”.

“Changamoto kubwa katika shughuli za Chuo ni jinsi ya kupanua miundombinu, kwa mfano,maktaba iliyopo pamoja na ukarabati mkubwa uliofanywa, bado ni ndogo sana kukidhi mahitaji ya wanafunzi na wahadhiri,” alisema Professa Mushi.

Alisema pia kuwa Chuo hicho kinachangamoto ya kuongeza au kuendeleza rasilimali watu kwani kwa sasa Chuo hicho kina wanataaluma 136 na kati ya hao,kumi tu ndiyo wana shahada ya udhamivu (PhD), 35 wana shahada ya udhamili na 91 wana shahada ya kwanza.

“Kwa kawaida wanataaluma wote wanaofundisha Chuo Kikuu wanatakiwa wawe na shada ya udhamivu,” aliongeza Professa Mushi.

Kufuatia hali hiyo,Professa Mushi alisema Chuo hicho kimekuwa kikiendesha shughuli zake kwa kuajiri wahadhiri wa muda wengi wao kutoka kampasi ya Mlimani ambapo mwaka jana pekee,wahadhiri wa muda walioajiriwa ni 147 na kukigharimu Chuo hicho zaidi ya Sh.milioni 600 fedha ambazo ni zaidi ya nusu ya fedha za matumizi mengineyo (OC) ya Chuo hicho.

Kaimu Mwenyekiti wa Baraza la Chuo Kikuu cha Dar-Es-Salaam,Jaji Joseph Warioba naye hakuwa na jingine zaidi ya kulalamikia miundombinu mibovu ya Chuo hicho cha Mkwawa ambaye aliiomba serikali kuongeza fungu la fedha la kusomesha wahadhiri katika Chuo Kikuu cha Mkwawa.

Jaji Warioba alisema ikiwezekana, ni vyema serikali ikabuni mpango mahsusi wa kusomesha wahadhiri wa Chuo Kikuu cha Mkwawa katika ngazi ya udhamili na udhamivu.

Jaji Warioba hata hivyo, aliipongeza serikali kwa kuanzisha Mpango wa Maendeleo ya Elimu ya Juu (MMEJU) Mpango ambao alisema utaiwezesha sekta ya elimu ya juu kuongeza mchango wake katika maendeleo ya Taifa.

Mikakati ya MUCE kukabiliana na Changamoto zake:

Kutokana na uchanga wa Chuo Kikuu cha Mkwawa na mazingira magumu wakati kilipoanzishwa, kumekuwepo na mikakati ya kukifanya kiwe na nyenzo zote za kutoa elimu bora ambapo imeanzishwa miradi mbalimbali ambayo ni pamoja na mradi wa ujenzi wa jengo la utawala,ofisi,kumbi za mihadhara na maabara za sayansi.

Mradi mwingine ni wa kuendeleza rasilimali watu, mwingine wa kupanua maktaba. Upo pia mradi wa kuongeza nafasi na idadi ya ofisi kwa ajili ya wafanyakazi, kuboresha mabweni ya wanafunzi, kukarabati miundombinu na mifumo ya maji, barabara,umeme,mawasiliano na kuboresha mazingira ya chuo.

Thursday, October 28, 2010

UPASUAJI WAOKOA MACHO YA WATU 33 IRINGA

Mratibu wa huduma za Afya ya macho na Daktari wa macho mkoani Iringa akimpima macho mgonjwa wa macho.Picha nyingine ni muuguzi akimfunga dawa mgonjwa aliyefanyiwa upasuaji na wengine ni wagonjwa waliofanyiwa upasuaji wa macho katika kituo cha Afya Malangali wilayani Mufindi hivi karibuni.

Tuesday, October 5, 2010

TUNADI SERA ZETU

Wagombea ubunge katika jimbo la Kalenga Mkoani Iringa kutoka kushoto na vyama vyao kwenye mabano ni John Katindasa (TLP), Rehema Makoga (Chadema) na Ismail Makuke (Jahazi Asilia) wakijibu maswali ya wapiga kura katika mdahalo wa wagombea na wapiga kura wa jimbo hilo uliofanyika kwenye ukumbi wa serikali ya kijiji.Mgombea wa CCM,Dk.William Mgimwa hakuwepo kwenye mdahalo kutokana marufuku ya CCM kwa wagombea wa ngazi zote kuhudhuria midahalo.

MGOMBEA WA UBUNGE KALENGA KUPITIA TLP AKIWA HANA LA KUFANYA

Mgombea wa Ubunge Jimbo la Kalenga,kupitia Chama cha TLP,John Katindasa (Mwenye suti nyeusi katikati) akiwa hana la kufanya baada ya gari lake kugoma kuwaka muda mfupi baada ya kumalizika kwa mdahalo wa wagombea na wapiga kura wa Jimbo la Kalenga.Wengine walioshiriki mdahalo huo ni Mgombea wa kupitia Chadema, Rehema Makoga na mgombea kutia Jahazi Asilia,Ismail Makuke.

Wednesday, September 22, 2010

MWAKALEBELA KATIKA MATUKIO TOFAUTI NA KIKWETE SAMORA JANA

Aliyeongoza katika kura za maoni,Frederick Mwakalebela jana katika uwanja wa Samora alishangiliwa kuliko hata Kikwete hali iliyoonesha dhahiri kwamba ni kipenzi cha wakati wa Jimbo la Iringa Mjini.Picha tatu tofauti zinaonesha Kikwete akimnadi Mwakalebelas katika ile hali ya kuvunja makundi na kutangaza rasmi kwamba anakiunga mkono Chama Cha Mapinduzi pamoja na mgombea wa Jimbo la Iringa Mjini,kupitia chama hicho,Monica Mbega.

Wednesday, September 15, 2010

Monday, September 13, 2010

VODACOM MISS TANZANIA 2010


VodaCom Miss Tanzania 2010,Genevieve Emmanuel Mpangala (Kati). Kushoto ni mshindi namba mbili,Glory Mwanga na mshindi wa tatu,Consolata Lucas.

Friday, September 10, 2010

Wednesday, September 8, 2010

JK ALIPOKUWA MORO


NCCR-MAGEUZI IRINGA KIKAAONGONI

MSIMAMIZI wa Uchaguzi Jimbo la Iringa Mjini,Theresia Mahongo amekitaka Chama cha NCCR-Mageuzi kuitisha mkutano wa hadhara kuwaomba radhi mgombea Ubunge wa Jimbo hilo kupitia Chadema,Mchungaji Peter Msigwa na Mjumbe wa Kamati Kuu ya Chadema,Chiku Abwao.

NCCR-Mageuzi pia imetakiwa kuandika barua ya kuwaomba radhi Mchugaji Msigwa na Abwao na nakala yake kutumwa kwa Msimamizi huyo wa Uchaguzi Jimbo la Iringa Mjini.

Agizo hilo la Msimamizi wa Uchaguzi Jimbo la Iringa kwa Chama cha NCCR-mageuzi limekuja siku tano baada ya wafuasi wa Mgombea wa Ubunge jimbo hilo kupitia Chama hicho cha NCCR-Mageuzi,Mariam Mwakingwe, kupanda jukwaani na kurusha matusi yasiyoandika katika mkutano wa kampeni uliofanyika Stendi ya Mabasi,Mjini Iringa,Agosti 31,mwaka huu.

Wafuasi hao ni Francis Blanka ambaye ni Katibu Mwenezi wa Chama cha Tanzania Labour (TLP) Mkoa wa Iringa na Benny Kapwani ambaye alikuwa Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Mkoa wa Iringa, kwa nyakati tofauti katika mkutano huo wa kampeni walipanda jukwaani na kuvurumisha matusi yasiyoandikika kwa mchungaji Msigwa na Abwao.

Kwa mujibu wa barua ya Mahongo ya Septemba 06,mwaka huu, kwenda kwa NCCR-Mageuzi ambayo Nipashe imepata nakala yake, Msimamizi huyo pia amekiagiza Chama hicho kuacha kumpeni za matusi vinginevyo kitatozwa faini ya Sh.100,000 au kufutwa kwenye kampeni hadi Oktoba 31,mwaka huu.

“Kwa mujibu wa kifungu cha 5:8 (a) cha maadili ya Uchaguzi, (NCCR) mnaagizwa kuomba radhi hadharani katika eneo lilelile mlilotumia kutoa lugha ya kashfa. Mnaagizwa kutuletea tarehe utakayofanya mkutano huo wa kuomba radhi ndani ya siku tatu ili Kamati ya Maadili ya Uchaguzi uhudhurie kwa ajili ya kujiridhisha,” ilisema sehemu ya barua hiyo.

Maagizo hayo kwa NCCR-Mageuzi yaliyotolewa na Msimamizi huyo wa Uchaguzi,yanafuatia kikao cha Maadili ya Uchaguzi kilichoketi Septemaba 04,mwaka huu kujadili malalamiko yaliyowasilishwa kwenye kamati hiyo na Mchugaji Msigwa pamoja na Abwao.

Barua ya malalamiko hayo iliyosainiwa na Katibu wa Chadema Iringa Mjini,Suzane Mgonakulima, iliitaka ofisi ya Msimamizi huyo kuchukua hatua mara moja kwa mujibu wa taratibu zilizowekwa ili kuepusha uvunjifu wa amani katika Jimbo hilo.

Katibu wa NCCR-Mageuzi Mkoa wa Iringa,James Mwamgiga amekiri kupokea barua ya msimamizi huyo lakini amesema hawataitekeleza na badala yake wamekata rufaa.

“Barua ile imekuja tofauti na tulivyokubalina kwenye kikao cha maadili, kuna maneno yameongezwa ikiwemo kuwaandikia (Mchungaji Msigwa na Abwao) barua ya kuwaomba radhi,..tunasubiri kwanza maamuzi ya rufani yetu,” alisema Mwamgiga.

Mwisho.

Wednesday, September 1, 2010

WAPINZANI IRINGA WAWEKA KANDO KAMPENI,WAANZA VITA YA MATUSI

Septemba 01:BAADHI ya wakazi wa Jimbo la Iringa mjini wamelaani vikali vitengo vya baadhi ya wafuasi wa wagombea wa ubunge wa jimbo hilo kuanza kampeni chafu za kurushiana matusi majukwaani.

Wananchi hao pia wametoa masikitiko na kuonyesha wasiwasi kama wafuasi hao wana nia njema na Jimbo hilo kutokana na kuacha kazi ya kueleza mikakati ya namna gani nzuri watakavyowahudumia wananchi na kutumia muda mrefu kutukanana.

Aidha, wananchi hao wamefikia hatua ya kuwalaani baada ya wafuasi wa Mgombea wa Ubunge Jimbo la Iringa Mjini kupitia unaojiita ‘Muungano wa Upinzani’, Mariam Mwakingwe kupanda jukwaani na kuanza kurusha matusi katika mkutano wa kampeni,Jumanne, Agosti 31,mwaka huu katika Stendi ya Mkoa wa Iringa.

Francis Blanka ambaye ni Katibu Mwenezi wa Chama cha Tanzania Labour (TLP) Mkoa wa Iringa na Benny Kapwani ambaye alikuwa Mwenyekiti wa Chma cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Mkoa wa Iringa, kwa nyakati tofauti jana walipanda jukwaani na kuvurumisha matusi yasiyoandikika.

Walikuwa wanamshambulia Mjumbe wa Kamati Kuu ya CHADEMA,Chiku Abwao, ambaye katika uzinduzi rasmi wa kampeni za CHADEMA Mkoa wa Iringa, alidai kuwa aliyekuwa Mwenyekiti wao (CHADEMA) Mkoa wa Iringa alijiuzulu wadhifa huo baada ya chake chake kubaini kuwa amenunuliwa na CCM ili kuwahujumu.

Mwingine aliyekuwa akiporomoshewa matusi hayo ni mgombea Ubunge wa Jimbo hilo kupitia CHADEMA,Mchungaji Peter Msigwa
Chiku alidai kuwa,wanazo taarifa kwamba Kapwani ambaye alikuwa amechukua fomu za kuwania ubunge Jimbo la Isimani hakurejesha fomu hizo kutokana na kununuliwa na mgombea mwingine ambaye amekuwa Mbunge wa Isimani kwa miaka 15 na ambaye kwa sasa ni Mkuu wa Mkoa wa Dar-es-Salaam,William Lukuvi,hivyo mgombea huyo wa CCM kupita bila kupingwa.

Ndipo vurugu zilipoanza ambapo jana Kapwani na Blanka walishirikiana kurusha matusi hayo kwa Abwao na Msigwa na kufanya baadhi ya watu waamini kuwa huenda watu hao walikuwa ‘wamechanganyikiwa’.

Wakizungumza kwa nyakati tofauti, baadhi ya wananchi waliohudhuria mkutano huo walisema wamesikitishwa na hali hiyo na kuitaka Serikali kupitia ofisi ya Tume ya Taifa ya Uchaguzi kuwaonya watu hao kama si kuwafuta kabisa kwenye kampeni.

“Tulikuja kusikia sera zao lakini kama tungejua kwamba tunakuja kusikia watu na heshima zao wakitukana hadharani wala tusingepoteza muda wetu,” alisema mkazi wa Ilala iliyetambulisha kwa jina la Elisha Mhanga.

Chiku Abwao mwenyewe aliiambia Blog hii baadaye kuwa alikuwa anakusanya ushahidi ili awasilishe kwa Msimamizi wa Uchaguzi wa Jimbo la Iringa Mjini kabla ya kufungua kesi mahakamani kwa sababu wazungumzaji walimshambulia yeye binafsi na biashara zake.

Msimamizi wa Uchaguzi wa Jimbo hilo,Theresia Mahongo alisema hakuwa amepata malalamiko yoyote lakini akavikumbusha vyama vya siasa kuzingatia maadili ya Uchaguzi waliyosaini vinginevyo watashughulikiwa.

“Binafsi sikuyasikia hayo matusi kwa sababu sikuwepo kwenye mkutano wao lakini nitafuatilia ili niwakumbushe kwamba kampeni siyo njia ya kuchochea uvunjifu wa mshikamano na amani tuliyonayo,” alisema Mahongo.

Umeibuka mpasuko mkubwa katika kambi ya upinzani Mjini Iringa mpasuko ambao ni dhahiri unaweza kumnufaisha mgombea Ubunge wa Jimbo hilo kupitia CCM,Monica Mbega ambaye naye ana wakati mgumu kutokana na mpasuko ndani ya CCM katika Jimbo hilo unaodaiwa kuwepo baada ya aliyeongoza katika kura za maoni,Frederick Mwakalebela, kuenguliwa na NEC ya CCM.

Katika kambi ya upinzani,vyama vya TLP,CUF,APPT na NCCR-Mageuzi vinamuunga mkono mgombea kupitia NCCR-Mageuzi,Mariam Mwakingwe huku CHADEMA wakiwa hawautambui muungano huo hali ambayo imeleta uhasama mkubwa na kuanza kushambulia peupe kwenye majukwaa ya kampeni.

Mwisho

Tuesday, August 31, 2010

LAPF YACHANGIA MFUKO WA WANAFUNZI MKWAWA


Meneja Mwandamizi wa Masoko na Mawasiliano wa LAPF akikabidhi hundi ya Sh.300,000/-kwa Naibu wa Mkuu wa Chuo Kikuu cha Mkwawa-MUCE, anayeshughulikia Utawala,Professa John Machiwa.
Fedha hizo ni mchango wa LAPF katika kutunisha mfuko wa zawadi za wanafunzi wanaofanya vizuri katika masomo yao Chuoni hapo.

CHUO KIKUU MKWAWA WATEMBEZA BAKULI KUOMBA MSAADA

Agosti 31:CHUO Kikuu kishiriki cha Elimu cha Mkwawa cha Mkoani Iringa (MUCE),kimeyalilia mashirika na wahisani mbalimbali kuliokoa jahazi la Chuo hicho ambalo limeelezwa kuwa linazama kila kukicha.

Akizungmza na ugeni wa Mfuko wa Pensheni wa Serikali za Mitaa (LAPF),uliotembelea Chuoni hapo leo (Agosti 31) Mwanasheria Mwandamizi wa Chuo hicho,Alfred Nyamwangi amesema Chuo hicho kinakabiliwa na changamoto nyingi zinazowafanya ustawi wa Chuo hicho uwe wa kusuasua.

Ugeni huo pamoja na mambo mengine, ulifika Chuo hapo kuchangia mfuko wa zawadi kwa wanafunzi wanaofanya vyema katika masomo yao zawadi ambazo hutolewa katika mahafali ya Chuo hicho.

Moja ya Changamoto hizo alisema na kushindwa kuwa na miundombinu ya kuwalaza wanafunzi wote Chuoni hapo na hivyo kuwafanya wanafunzi wengi kuishi maeneo ya hatari.

Alisema miundombinu inayotumika ni ile iliyokuwa inatumika wakati ikiwa ni Shule ya sekondari ya Mkwawa.

Alisema mabweni waliyonayo, kwa mfano, yana uwezo wa kulaza wanafunzi 1060 ikiwa ni chini ya asilimia 60 ya wanafunzi wote. Chuo hicho kwa sasa kina zaidi ya wanafunzi 1,900.

Aidha, alisema hakuna jengo la utawala na kwamba wahadhiri wamekuwa wakitumia ofisi zilizokuwa za walimu wa sekondari.

“Kimsingi hatuna ofisi hata moja vivyo hivyo jengo la Utawala na hali hii imekuwa inatishia ustawi wa Chuo chetu,” alisema Nyamwangi.
Alisema Chuo hicho kinahitaji kumbi nne za mihadhara na kwamba moja ndiyo kwanza imeanza kujengwa kwa fedha za serikali na nyingine inaweza kuanza kujengwa mwakani kwa ufadhili wa Benki ya Dunia.

Kufuatia Changumoto hizo,Nyamwangi aliiomba LAPF kutumia mfumo wa Jengo, Tumia na Hamisha ambapo inaweza kuingia mkataba na Chuo hicho, ikapewa eneo la kujenga na baada ya miaka kadhaa majengo hayo yakamilikishwa kwa Chuo hicho.

Akizungumza mara baada ya kukabidhi hundi ya Sh.laki tatu kwa uongozi wa MUCE,Meneja Mwandamizi wa Masoko na Mawasiliano wa LAPF,Andrew Kuyeyana alisema licha ya kitoa kiasi hicho kidogo cha fedha kwenye mfuko wa kuwamotisha wanafunzi wa Chuo hicho, LAPF itaendelea kuchangia kwenye mfuko huo kila mwaka.

Aliuomba uongozi wa MUCE wakutane na uongozi wa LAPF ili kuona ni namna gani nzuri ya kusaidiana kutatua changamoto zinazokikabili Chuo hicho.

Aidha,Naibu Makamu wa Mkuu wa Chuo hicho, anayeshughulikia Utawala,Professa John Machiwa aliishukuru LAPF kwa kutambua umuhimu wa kuwamotisha wanafunzi lakini pia kuonyesha nia ya kuchangia katika kutatua changamoto za Chuo hicho.

Monday, August 30, 2010

JK ANAPOGOMBANIWA NA WAPIGA KURA!


JK akigombaniwa na wapigakura huko Sumbawanga a.k.a Mjini Tupa uchawi

CHADEMA WAJINUFAISHA NA MGOGORO WA CCM

Agosti 30: CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Mkoa wa Iringa jana (Agosti 30) kimezindua rasmi kampeni zake huku kikitumia mpasuko wa CCM katika Manispaa ya Iringa kama mtaji wake mkubwa.

CCM Manispaa ya Iringa kinadaiwa kuwa na mpasuko unaodaiwa kuwepo baada ya Halmashauri Kuu ya CCM (NEC) kumwengua Frederick Mwakalebela licha ya kuongoza katika kura za maoni na kumweka aliyeshika nafasi ya pili,Monica Mbega ambaye pia alikuwa Mbunge wa jimbo hilo.

Akizungumza katika mkutano wa kampeni katika viwanja vya Mwembetogwa, Manispaa ya Iringa, Mgombea wa CHADEMA,Mchugaji Peter Msigwa aliwaomba wanachama na wafuasi wa CCM kumkataa mgombea wa chama hicho,Monica Mbega kwa sababu siyo chaguo lao.

Msigwa huku akishangiliwa na maelfu ya wananchi waliohudhuria mkutano huo wa kampeni, alisema imekuwa ni kawaida kwa CCM kuwachagulia wananchi mgombea na kuwataka wananchi wa jimbo la Iringa Mjini kutodanganyika.

“Kwa niaba ya familia yangu na kwa niaba ya chama changu (CHADEMA), tunampa pole sana Mwakalebela kwa kuonewa na NEC ya CCM lakini tunawaomba wananchi wa Iringa, mfuteni machozi ndugu yetu huyu (Mwakalebela) kwa kuinyima kura CCM,” alisema Mchungaji Msigwa.

Mchungaji Msigwa ambaye uchaguzi wa mwaka 2005 aligombea jimbo hilo kupitia chama cha Tanzania Labour (TLP) alisema endapo atachaguliwa atawatumikia wananchi wa Manispaa ya Iringa kwa unyenyekevu mkubwa kwa sababu wao ndiyo waajiri wake.

Alisema atatumia vitivo mbalimbali vya Vyuo Vikuu vilivyopo Manispaa ya Iringa kuviunganisha na wananchi katika harakati ya kuvitumia Vyuo hivyo kuleta maendeleo.

Wengine waliohudhuria uzinduzi huo ni pamoja na aliyekuwa kada wa CCM ambaye ametimkia CHADEMA na anagombea Jimbo la Njombe Kaskazini,Alatanga Nyagawa.

Nyagawa alijinasibu kuwa yeye, msigwa pamoja na aliyekuwa kada mwingine wa CCM aliyetimkia Chadema,Thomas Nyimbo tayari ni wabunge kutokana na kile alichokieleza kuwa wapinzania wao ni dhaifu.

“Tutatumia udhaifu wa wagombea wenzetu kushinda kwa kishindo,” alisema.

Moja ya udhaifu wa mgombea wa CCM katika jimbo la Njombe Kaskazini ambaye pia ni Mwenyekiti wa CCM Mkoa Iringa,Deo Sanga maarufu Jah People,ni kudaiwa kuwa na elimu ya darasa la pili.

“Nitawaomba wananchi wa Njombe Kaskazini wamnyime kura Deo Sanga ili arudi MEMKWA (mpango maalum wa elimu kwa walioikosa),” alisema.

Hata hivyo,Sanga mwenyewe alipoongea na BLOG HII kwa simu alikanusha madai kwamba elimu yake ni darasa la pili bali akasema elimu yake ni darasa la saba na kwamba alisoma katika shule ya msingi Ikwega iliyopo wilayani Mufindi, ingawa alisema hakumbuki alihitimu mwaka gani.

“Mpaka nirejee kwenye kumbukumbu zangu ndiyo naweza kukueleza nilianza mwaka gani na nikamaliza mwaka gani,” alisema Deo Sanga, hata hivyo alipotafutwa baadaye alikuwa hapatikani.

Hata hivyo, alisema Nyagawa anayedai kwamba yeye (Sanga) ni mbumbumbu ni mfa maji anayetapatapa baada ya kuangushwa katika kura za maoni za CCM na kukumbilia CHADEMA.

WAODAI STAKABADHI KUBANWA NA SHERIA

Agosti 30:MAMLAKA ya Mapato (TRA) Mkoa wa Iringa imewatahadharisha wananchi kuwa watakumbana na mkono wa sheria ikiwa wataendelea kununua bidhaa mbalimbali bila kudai sitakabadhi ya manunuzi yao.

Akizungumza na blog hii ofisini kwake,Menaja wa TRA Mkoa wa Iringa,Rosalia Mwenda alisema sheria iliyowezesha kuwepo kwa mashine maalumu za kielektroniki (EFD) za kutoa stakabadhi na kutunza kumbukumbu, inambana pia mnunuzi kudai risiti kwa kila bidhaa anayouziwa.

Kwa mujibu wa Meneja huyo, sheria hiyo inawataka wafanyabiashara wote walioandikishwa na kodi ya ongezeko la thamani (VAT) kufunga mashine hizo kwenye maeneo yao ya biashara.

“Moja ya vikwazo vya kukusanya kodi ambavyo vimetukabili muda mrefu ni wananchi kutokuwa na utamaduni wa kudai syakabadhi, kwa bahati nzuri sheria ya mashine hizi za EFD inambana pia mtu ambaye atakuwa na bidhaa lakini akiwa hana stakabadhi, hivyo tunaomba wananchi kila wanaponunua bidhaa wadai stakabadhi vinginevyo watashitakiwa mahakamani” alisema.

Alisema EFD (Electronic Fiscal Device) ni mashine ambayo hutoa stakabadhi na kutunza kumbukumbu za kibiashara kwa muda wa miaka mitano na pia zitakuwa zinatoa taarifa TRA juu shughuli zote za kibiashara zinazofanywa na mfanyabiashara mwenye mashine hiyo kwa njia ya kielektroniki.

Alisema mwaka huu wa fedha yaani kuanzia Julai, 2010 hadi Juni 2011 TRA Mkoa wa Iringa imepangiwa kukusanya zaidi ya Sh.bilioni 23.112 ikiwa ni ongezeko la asilimia 32 ikilinganishwa na lengo la mwaka wa fedha wa 2009/2010.

Alisema mwaka wa fedha wa 2009/2010 walipangiwa kukusanya Sh.bilioni 16.773 lakini wakavuka lengo kwa kukusanya Sh.bilioni 17.663 sawa na asilimia 105 ya lengo.

Mwenda alisema waliweza kuvuka lengo kutokana na mikakati waliyojiwekea na kuitekeleza vyema ikiwa ni pamoja na kuweza kutekeleza shughuli ya ukaguaji wa hesabu za walipakodi hali iliyowaongezea makusanyo ya kodi.

Mkakati mwingine ni ukusanyaji kodi kwa vitalu, yaani maafisa wa TRA wamekuwa na utaratibu wa kuangalia hali halisi ya baishara za wafanyabiashara ikilinganishwa na nyuma ambapo wafanyabiashara wenyewe ndiyo walikuwa wanatamka kiwango cha mtaji walichonacho na kukadiriwa kodi.

Alisema elimu kwa mlipakodi imewasaidia pamoja na ushirikiano miongoni mwa wafanyakazi imekuwa ni chachu hiyo ya kuvuka lengo.

Sunday, August 29, 2010

MWAMUZI WEBB WA UINGEREZA ALIPOCHEMSHA SAUZI


De Jong wa timu ya Taifa ya Uholanzi akimrushia daluga Alonso wa timu ya Taifa ya Uhispania.
Mwamuzi aliyechezesha mechi hiyo ya fainali kule kwa mzee wetu Madiba, muingereza Howard Webb amekiri kuwa,De Jong alistahili kadi nyekudu badala ya njano aliyompa.
Chonde chonde waamuzi, kuwenu makini ili tufaidi burudani hii ya dunia.

Friday, August 27, 2010

TLP IRINGA WATIMULIWA KWENYE JENGO

CHAMA cha Tanzania Labour (TLP) Mkoa wa Iringa, kimepata pigo baada ya ofisi yake kufungwa na samani zote za ofisi hiyo kushikiliwa kwa ajili ya kupigwa mnada na kampuni ya udalali ya Majembe.

TLP iliyokuwa imeweka Ofisi zake katika jengo la Akiba House linalomilikiwa na Shirika la Hifadhi ya Jamii (NSSF) hadi sasa haina Ofisi na hivyo kuwafanya viongozi wake kuhaha mitaani.

Ofisi hiyo ilivunjwa juzi na vifaa vyote kuchukuliwa na Kampuniya Majembe ikiwemo mafaili na nyaraka mbalimbali kutoka na Chama hicho kudaiwa pango la zaidi ya Shilingi 2,400,000.

Jana mchana Nipashe iliwashuhudia watumishi wa kampuni ya udalali ya majembe wakiondoa samani za ofisi hiyo na kuzipakia kwenye magari yao na kisha kuifunga ofisi hiyo kwa makufuli maalumu.

Katibu wa TLP Mkoa wa Iringa, Mrisho Samson na Katibu Mwenezi wa Mkoa huo Francis Blanka walifika baadaye ofisini hapo na kujaribu kuoko baadhi ya nyaraka lakini walikataliwa na wafanyakazi hao wa Majembe.

Meneja wa Operesheni wa Majembe, Mussa Moto hakutaka kuzungumzia suala hilo kwa madai kwamba jambo hilo waulizwe NSSF ndiyo waliowapa kazi hiyo ya kuwatoa baadhi ya wapangaji.

Kwa upande wake,Meneja wa NSSF Mkoa wa Iringa, Bathow Mmuni, alisema hawakuwa na lengo lolote la kisiasa dhidi ya TLP bali wako kwenye operesheni ya kukusanya madeni kutoka kwa wadaiwa sugu.

Alisema TLP ni mmoja wa wapangaji ambao ni wadaiwa sugu katika jengo hilo la ‘Akiba House’ na kwamba hawakuwa na njia mbadala bali ni kuwaondoa kwenye jengo kutokana na kushindwa kulipa kodi kwa zaidi ya miaka miwili.

Alisema katika operesheni hiyo,jumla ya wapangaji 33 waliopo kwenye majengo mbalimbali ya vitega uchumi vya NSSF Mkoani Iringa, walikuwa ni wadaiwa sugu ambapo baada ya shughuli hiyo ya kukusanya madeni kukabidhiwa kwa Majembe Auction Mart,zaidi ya Sh.milioni 54.5 zimekusanya.

Alisema wapamgaji tisa wakiwemo TLP ambao wameshindwa kulipa madeni, wameondolewa kwa nguvu na mali zao hususani samani za ofisi zimetaifishwa mpaka watakapolipa madeni na wakishindwa samani hizo zitauzwa kwa mnada.

Katibu wa Mkoa wa TLP,Samson hakutaka kulizungumzia suala hilo kwa maelezo kuwa siyo msemaji lakini Katibu Mwenezi,Blanka alikiri TLP kudaiwa Sh.2,400,000 ikiwa ni kodi ya pango.

Hata hivyo, alisema Chama chake (TLP) Taifa kimeshakiri kulitambua deni hilo na walikuwa wameandika barua kwa NSSF kwamba watachelewa kidogo kulipa kwa sababu Mwenyekiti wa Taifa,Agustino Mrema ambaye alipaswa kusaini hundi ya malipo hayupo Dar-es-Salaam.

Mrema Mwenyewe alipopigiwa Simu alijibu kwa kifupi tu kisha kukata simu: “Mimi nahangaikia Jimbo langu la Vunjo bwana hayo mambo ya ofisi siyajuwi”.

TLP ni moja ya vyama vya upinzani vilivyosimamisha wagombea wa ubunge katika Jimbo la Kalenga na katika majimbo mengine kimekuwa pega kwa pega kuwaunga mkono wagombea wengine wa vyama vya upizani na sasa kimetaifishwa ofisi ya kuratibu shughuli hizo za kampeni.

Tuesday, August 24, 2010

HILI SIYO BANDA LA KUKU NI BWENI!

Wanafunzi wapatao 100 wa shule ya sekondari ya Bomalang'ombe wilayani Kilolo inayomilikiwa na Kanisa la Kiinjili la Kilutheri nchini (KKKT) Dayosisi ya Iringa walikuwa wakilitumia 'kujisomea' usiku na wakilala humu kabla waumini wa kanisa hilo wa nchini marekani hawajatoa fedha kwa ya ujenzi wa bweni zuri. Jiulize Mwenyewe,mwanafunzi anayejisomea kwenye bweni hili na kulala humo, atafaulu mtihani wake wa kidato cha nne?.

Tafakari,Chukua hatua!

Wageni waliofika kujionea Bweni lililojengwa kwa kutumia mabaki ya magogo ya mbao maarufu 'mabanzi' wengi wao kutoka Marekani.
Wageni hawa pamoja na mambo mengine,walifika kujionea bweni hilo pia kushuhudia uzinduzi wa bweni la heshima la utu lililojengwa kwa ufadhili wa fedha zao ili kuwaokoa wanafunzi waliokuwa wakilala kwenye bweni hilo la mateso makubwa.