McEddy Elroy

Wednesday, September 22, 2010

MWAKALEBELA KATIKA MATUKIO TOFAUTI NA KIKWETE SAMORA JANA

Aliyeongoza katika kura za maoni,Frederick Mwakalebela jana katika uwanja wa Samora alishangiliwa kuliko hata Kikwete hali iliyoonesha dhahiri kwamba ni kipenzi cha wakati wa Jimbo la Iringa Mjini.Picha tatu tofauti zinaonesha Kikwete akimnadi Mwakalebelas katika ile hali ya kuvunja makundi na kutangaza rasmi kwamba anakiunga mkono Chama Cha Mapinduzi pamoja na mgombea wa Jimbo la Iringa Mjini,kupitia chama hicho,Monica Mbega.

Wednesday, September 15, 2010

Monday, September 13, 2010

VODACOM MISS TANZANIA 2010


VodaCom Miss Tanzania 2010,Genevieve Emmanuel Mpangala (Kati). Kushoto ni mshindi namba mbili,Glory Mwanga na mshindi wa tatu,Consolata Lucas.

Friday, September 10, 2010

Wednesday, September 8, 2010

JK ALIPOKUWA MORO


NCCR-MAGEUZI IRINGA KIKAAONGONI

MSIMAMIZI wa Uchaguzi Jimbo la Iringa Mjini,Theresia Mahongo amekitaka Chama cha NCCR-Mageuzi kuitisha mkutano wa hadhara kuwaomba radhi mgombea Ubunge wa Jimbo hilo kupitia Chadema,Mchungaji Peter Msigwa na Mjumbe wa Kamati Kuu ya Chadema,Chiku Abwao.

NCCR-Mageuzi pia imetakiwa kuandika barua ya kuwaomba radhi Mchugaji Msigwa na Abwao na nakala yake kutumwa kwa Msimamizi huyo wa Uchaguzi Jimbo la Iringa Mjini.

Agizo hilo la Msimamizi wa Uchaguzi Jimbo la Iringa kwa Chama cha NCCR-mageuzi limekuja siku tano baada ya wafuasi wa Mgombea wa Ubunge jimbo hilo kupitia Chama hicho cha NCCR-Mageuzi,Mariam Mwakingwe, kupanda jukwaani na kurusha matusi yasiyoandika katika mkutano wa kampeni uliofanyika Stendi ya Mabasi,Mjini Iringa,Agosti 31,mwaka huu.

Wafuasi hao ni Francis Blanka ambaye ni Katibu Mwenezi wa Chama cha Tanzania Labour (TLP) Mkoa wa Iringa na Benny Kapwani ambaye alikuwa Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Mkoa wa Iringa, kwa nyakati tofauti katika mkutano huo wa kampeni walipanda jukwaani na kuvurumisha matusi yasiyoandikika kwa mchungaji Msigwa na Abwao.

Kwa mujibu wa barua ya Mahongo ya Septemba 06,mwaka huu, kwenda kwa NCCR-Mageuzi ambayo Nipashe imepata nakala yake, Msimamizi huyo pia amekiagiza Chama hicho kuacha kumpeni za matusi vinginevyo kitatozwa faini ya Sh.100,000 au kufutwa kwenye kampeni hadi Oktoba 31,mwaka huu.

“Kwa mujibu wa kifungu cha 5:8 (a) cha maadili ya Uchaguzi, (NCCR) mnaagizwa kuomba radhi hadharani katika eneo lilelile mlilotumia kutoa lugha ya kashfa. Mnaagizwa kutuletea tarehe utakayofanya mkutano huo wa kuomba radhi ndani ya siku tatu ili Kamati ya Maadili ya Uchaguzi uhudhurie kwa ajili ya kujiridhisha,” ilisema sehemu ya barua hiyo.

Maagizo hayo kwa NCCR-Mageuzi yaliyotolewa na Msimamizi huyo wa Uchaguzi,yanafuatia kikao cha Maadili ya Uchaguzi kilichoketi Septemaba 04,mwaka huu kujadili malalamiko yaliyowasilishwa kwenye kamati hiyo na Mchugaji Msigwa pamoja na Abwao.

Barua ya malalamiko hayo iliyosainiwa na Katibu wa Chadema Iringa Mjini,Suzane Mgonakulima, iliitaka ofisi ya Msimamizi huyo kuchukua hatua mara moja kwa mujibu wa taratibu zilizowekwa ili kuepusha uvunjifu wa amani katika Jimbo hilo.

Katibu wa NCCR-Mageuzi Mkoa wa Iringa,James Mwamgiga amekiri kupokea barua ya msimamizi huyo lakini amesema hawataitekeleza na badala yake wamekata rufaa.

“Barua ile imekuja tofauti na tulivyokubalina kwenye kikao cha maadili, kuna maneno yameongezwa ikiwemo kuwaandikia (Mchungaji Msigwa na Abwao) barua ya kuwaomba radhi,..tunasubiri kwanza maamuzi ya rufani yetu,” alisema Mwamgiga.

Mwisho.

Wednesday, September 1, 2010

WAPINZANI IRINGA WAWEKA KANDO KAMPENI,WAANZA VITA YA MATUSI

Septemba 01:BAADHI ya wakazi wa Jimbo la Iringa mjini wamelaani vikali vitengo vya baadhi ya wafuasi wa wagombea wa ubunge wa jimbo hilo kuanza kampeni chafu za kurushiana matusi majukwaani.

Wananchi hao pia wametoa masikitiko na kuonyesha wasiwasi kama wafuasi hao wana nia njema na Jimbo hilo kutokana na kuacha kazi ya kueleza mikakati ya namna gani nzuri watakavyowahudumia wananchi na kutumia muda mrefu kutukanana.

Aidha, wananchi hao wamefikia hatua ya kuwalaani baada ya wafuasi wa Mgombea wa Ubunge Jimbo la Iringa Mjini kupitia unaojiita ‘Muungano wa Upinzani’, Mariam Mwakingwe kupanda jukwaani na kuanza kurusha matusi katika mkutano wa kampeni,Jumanne, Agosti 31,mwaka huu katika Stendi ya Mkoa wa Iringa.

Francis Blanka ambaye ni Katibu Mwenezi wa Chama cha Tanzania Labour (TLP) Mkoa wa Iringa na Benny Kapwani ambaye alikuwa Mwenyekiti wa Chma cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Mkoa wa Iringa, kwa nyakati tofauti jana walipanda jukwaani na kuvurumisha matusi yasiyoandikika.

Walikuwa wanamshambulia Mjumbe wa Kamati Kuu ya CHADEMA,Chiku Abwao, ambaye katika uzinduzi rasmi wa kampeni za CHADEMA Mkoa wa Iringa, alidai kuwa aliyekuwa Mwenyekiti wao (CHADEMA) Mkoa wa Iringa alijiuzulu wadhifa huo baada ya chake chake kubaini kuwa amenunuliwa na CCM ili kuwahujumu.

Mwingine aliyekuwa akiporomoshewa matusi hayo ni mgombea Ubunge wa Jimbo hilo kupitia CHADEMA,Mchungaji Peter Msigwa
Chiku alidai kuwa,wanazo taarifa kwamba Kapwani ambaye alikuwa amechukua fomu za kuwania ubunge Jimbo la Isimani hakurejesha fomu hizo kutokana na kununuliwa na mgombea mwingine ambaye amekuwa Mbunge wa Isimani kwa miaka 15 na ambaye kwa sasa ni Mkuu wa Mkoa wa Dar-es-Salaam,William Lukuvi,hivyo mgombea huyo wa CCM kupita bila kupingwa.

Ndipo vurugu zilipoanza ambapo jana Kapwani na Blanka walishirikiana kurusha matusi hayo kwa Abwao na Msigwa na kufanya baadhi ya watu waamini kuwa huenda watu hao walikuwa ‘wamechanganyikiwa’.

Wakizungumza kwa nyakati tofauti, baadhi ya wananchi waliohudhuria mkutano huo walisema wamesikitishwa na hali hiyo na kuitaka Serikali kupitia ofisi ya Tume ya Taifa ya Uchaguzi kuwaonya watu hao kama si kuwafuta kabisa kwenye kampeni.

“Tulikuja kusikia sera zao lakini kama tungejua kwamba tunakuja kusikia watu na heshima zao wakitukana hadharani wala tusingepoteza muda wetu,” alisema mkazi wa Ilala iliyetambulisha kwa jina la Elisha Mhanga.

Chiku Abwao mwenyewe aliiambia Blog hii baadaye kuwa alikuwa anakusanya ushahidi ili awasilishe kwa Msimamizi wa Uchaguzi wa Jimbo la Iringa Mjini kabla ya kufungua kesi mahakamani kwa sababu wazungumzaji walimshambulia yeye binafsi na biashara zake.

Msimamizi wa Uchaguzi wa Jimbo hilo,Theresia Mahongo alisema hakuwa amepata malalamiko yoyote lakini akavikumbusha vyama vya siasa kuzingatia maadili ya Uchaguzi waliyosaini vinginevyo watashughulikiwa.

“Binafsi sikuyasikia hayo matusi kwa sababu sikuwepo kwenye mkutano wao lakini nitafuatilia ili niwakumbushe kwamba kampeni siyo njia ya kuchochea uvunjifu wa mshikamano na amani tuliyonayo,” alisema Mahongo.

Umeibuka mpasuko mkubwa katika kambi ya upinzani Mjini Iringa mpasuko ambao ni dhahiri unaweza kumnufaisha mgombea Ubunge wa Jimbo hilo kupitia CCM,Monica Mbega ambaye naye ana wakati mgumu kutokana na mpasuko ndani ya CCM katika Jimbo hilo unaodaiwa kuwepo baada ya aliyeongoza katika kura za maoni,Frederick Mwakalebela, kuenguliwa na NEC ya CCM.

Katika kambi ya upinzani,vyama vya TLP,CUF,APPT na NCCR-Mageuzi vinamuunga mkono mgombea kupitia NCCR-Mageuzi,Mariam Mwakingwe huku CHADEMA wakiwa hawautambui muungano huo hali ambayo imeleta uhasama mkubwa na kuanza kushambulia peupe kwenye majukwaa ya kampeni.

Mwisho