Habari ndugu wapenzi wa Blog hii muipendayo.
Nasikitika kutoa taarifa kwamba,watu wasiofahamika wameingia ofisini kwangu kwa kutumia Master Keys na kuiba Computer yangu ndogo aina ya Apple na sasa imekuwa ngumu kuwa hewani mara kwa mara kwa sababu ya tatizo hilo.
Hizi huu umenistua sana hususani ikizingatiwa kwamba, wameingia na kuchukua Laptop tu hali inayonipa mashaka kama kweli walikuwa wanatafuta hiyo Laptop au wanatafuta kilichomo kwenye Laptop hiyo.
Pale mezani ilipokuwa Laptop,kulikuiwepo vitu vingi vyenye thamani kubwa kama Mordem ya Internet,Dvcam Camera yenye thamani ya dola za kimarekani 4,000, simu ya mkononi aina ya Nokia ambayo hata hivyo ni mbovu kidogo na ndiyo maana ilikuwa inabaki ofisini,kulikuwa pia na flash mbili moja ya GB mbili na nyingine ya MB 250 na vitu vingine vingi vidogo vidogo ambavyo nina uhakika kama ni vibaka wa kawaida wangevikusanya!.
Nashawishika kuamini kwamba kuna watu walikuwa wananifuatilia hasa baada ya kuwa nimeanza kuichunguza taasisi moja kubwa hapa mkoani Iringa ambayo baadhi ya viongozi na watumishi wake wana tuhuma nzito za ubadhilifu wa fedha za umma.
Nimetoa taarifa Polisi na kupewa RB Na.IR/RB/1666/2011 ya Machi 25,mwaka huu.Naomba dua zenu ili niweze kuipata Computer hiyo na kama kuna watu wananifuatilia, basi wasifanikiwe kunidhuru.
Hata hivyo,nawaahidi wapenzi wangu kwamba pamoja na tatizo hili nitaendelea kuwaletea vitu mlivyozoea hususani taarifa za uchunguzi bila woga wala upendeleo.
Tuko pamoja.!
McEddy Elroy
Showing posts with label Ufisadi Iringa. Show all posts
Showing posts with label Ufisadi Iringa. Show all posts
Sunday, March 27, 2011
Friday, August 13, 2010
MHASIBU WAKALA WA MAJENZI CORKOTINI
Na Mawazo Malembeka,Iringa
Agosti 13: MHASIBU Msaidizi wa Wakala wa Majenzi (TBA) Mkoa wa Iringa,Benjamin Mbope (56),amepandishwa kizimbani kwa makosa 94 ya kula njama, kughushi na kuibia wakala hao zaidi ya Sh.35.3
Mhasibu huyo msaidizi amefikishwa mahakamani jana (Agosti 12) katika mahakama ya wilaya ya Iringa.
Mbele ya Hakimu wa mahakama hiyo,Festo Lwila,Mwendesha mashitaka,Mrakibu msaidizi wa polisi,Matiku, alidai kuwa, kati ya Disemba 2, mwaka jana na Juni 8,mwaka huu, mtuhumiwa alitenda makosa hayo.
Matiku alidai kuwa, Desemba 2 mwaka jana, kwa nia ya kuidhulumu wakala hiyo, mtuhumiwa alikula njama na watu wasiojulikana na kuiba jumla ya Sh.35,377,300.
Aidha, Matiku aliendelea kuieleza mahakama hiyo kwamba, Desemba 23, mwaka jana, mtuhumiwa alighushi saini ya Meneja wa Wakala hiyo, Bartazar Kimangano na kuiba Sh.1,780,300 huku akijua kuwa ni kosa la jinai.
Mahakama hiyo iliendelea kuelezwa kwamba, Mhasibu huyo msaidizi aliandaa na hatimaye kuandika cheki yenye namba 3896729 na kuiba kiasi hicho cha fedha kutoka kwenye akaunti ya wakala hiyo yenye namba 01J1027842011 iliyopo benki ya CRDB Mkoa wa Iringa.
Katika kosa la kumi hadi 94, ilielezwa mahakamani hapo kwamba kati ya Disemba mwaka jana na Juni mwaka huu, mtuhumiwa huyo kwa nyakati tofauti alikuwa akiandaa hati za malipo na kuandika cheki na kuiba viwango tofauti tofauti cha fedha kinachofikia zaidi ya Sh.milioni 35.3.
Upande wa mashitaka ulisema dhamana kwa mtuhumiwa iko wazi ikiwa mtuhumiwa angetimiza masharti yatakayowekwa na mahakama.
Akisoma masharti ya dhamana, hakimu Lwila alisema mtuhumiwa alitakiwa kuwa na wadhamini wawili ambao kila mmoja amdhamini mtuhumiwa kwa Sh.milioni 40 na kwamba mmoja wa wadhamini hao lazima awe na mali isiyohamishika katika Manispaa ya Iringa, yenye thamani ya Sh.milioni 30.
Mtuhumiwa alishindwa kutimiza masharti ya dhamana na alipelekwa gereza la mahabusu hadi Agosti 26,shauri hilo litakapolejeshwa mahakamani hapo kwa kutajwa.
Mwisho.
Agosti 13: MHASIBU Msaidizi wa Wakala wa Majenzi (TBA) Mkoa wa Iringa,Benjamin Mbope (56),amepandishwa kizimbani kwa makosa 94 ya kula njama, kughushi na kuibia wakala hao zaidi ya Sh.35.3
Mhasibu huyo msaidizi amefikishwa mahakamani jana (Agosti 12) katika mahakama ya wilaya ya Iringa.
Mbele ya Hakimu wa mahakama hiyo,Festo Lwila,Mwendesha mashitaka,Mrakibu msaidizi wa polisi,Matiku, alidai kuwa, kati ya Disemba 2, mwaka jana na Juni 8,mwaka huu, mtuhumiwa alitenda makosa hayo.
Matiku alidai kuwa, Desemba 2 mwaka jana, kwa nia ya kuidhulumu wakala hiyo, mtuhumiwa alikula njama na watu wasiojulikana na kuiba jumla ya Sh.35,377,300.
Aidha, Matiku aliendelea kuieleza mahakama hiyo kwamba, Desemba 23, mwaka jana, mtuhumiwa alighushi saini ya Meneja wa Wakala hiyo, Bartazar Kimangano na kuiba Sh.1,780,300 huku akijua kuwa ni kosa la jinai.
Mahakama hiyo iliendelea kuelezwa kwamba, Mhasibu huyo msaidizi aliandaa na hatimaye kuandika cheki yenye namba 3896729 na kuiba kiasi hicho cha fedha kutoka kwenye akaunti ya wakala hiyo yenye namba 01J1027842011 iliyopo benki ya CRDB Mkoa wa Iringa.
Katika kosa la kumi hadi 94, ilielezwa mahakamani hapo kwamba kati ya Disemba mwaka jana na Juni mwaka huu, mtuhumiwa huyo kwa nyakati tofauti alikuwa akiandaa hati za malipo na kuandika cheki na kuiba viwango tofauti tofauti cha fedha kinachofikia zaidi ya Sh.milioni 35.3.
Upande wa mashitaka ulisema dhamana kwa mtuhumiwa iko wazi ikiwa mtuhumiwa angetimiza masharti yatakayowekwa na mahakama.
Akisoma masharti ya dhamana, hakimu Lwila alisema mtuhumiwa alitakiwa kuwa na wadhamini wawili ambao kila mmoja amdhamini mtuhumiwa kwa Sh.milioni 40 na kwamba mmoja wa wadhamini hao lazima awe na mali isiyohamishika katika Manispaa ya Iringa, yenye thamani ya Sh.milioni 30.
Mtuhumiwa alishindwa kutimiza masharti ya dhamana na alipelekwa gereza la mahabusu hadi Agosti 26,shauri hilo litakapolejeshwa mahakamani hapo kwa kutajwa.
Mwisho.
Subscribe to:
Posts (Atom)