McEddy Elroy

Sunday, March 27, 2011

WATU WANAONIFUATILIA WAIBA LAPTOP YANGU

Habari ndugu wapenzi wa Blog hii muipendayo.
Nasikitika kutoa taarifa kwamba,watu wasiofahamika wameingia ofisini kwangu kwa kutumia Master Keys na kuiba Computer yangu ndogo aina ya Apple na sasa imekuwa ngumu kuwa hewani mara kwa mara kwa sababu ya tatizo hilo.

Hizi huu umenistua sana hususani ikizingatiwa kwamba, wameingia na kuchukua Laptop tu hali inayonipa mashaka kama kweli walikuwa wanatafuta hiyo Laptop au wanatafuta kilichomo kwenye Laptop hiyo.

Pale mezani ilipokuwa Laptop,kulikuiwepo vitu vingi vyenye thamani kubwa kama Mordem ya Internet,Dvcam Camera yenye thamani ya dola za kimarekani 4,000, simu ya mkononi aina ya Nokia ambayo hata hivyo ni mbovu kidogo na ndiyo maana ilikuwa inabaki ofisini,kulikuwa pia na flash mbili moja ya GB mbili na nyingine ya MB 250 na vitu vingine vingi vidogo vidogo ambavyo nina uhakika kama ni vibaka wa kawaida wangevikusanya!.

Nashawishika kuamini kwamba kuna watu walikuwa wananifuatilia hasa baada ya kuwa nimeanza kuichunguza taasisi moja kubwa hapa mkoani Iringa ambayo baadhi ya viongozi na watumishi wake wana tuhuma nzito za ubadhilifu wa fedha za umma.

Nimetoa taarifa Polisi na kupewa RB Na.IR/RB/1666/2011 ya Machi 25,mwaka huu.Naomba dua zenu ili niweze kuipata Computer hiyo na kama kuna watu wananifuatilia, basi wasifanikiwe kunidhuru.

Hata hivyo,nawaahidi wapenzi wangu kwamba pamoja na tatizo hili nitaendelea kuwaletea vitu mlivyozoea hususani taarifa za uchunguzi bila woga wala upendeleo.

Tuko pamoja.!

No comments:

Post a Comment