McEddy Elroy

Tuesday, July 20, 2010

MAKADA WA CCM WAKANYAGANA UBUNGE IRINGA

Julai 20:HARAKATI za kuwania ubunge zinaonekana kuwa kali baada ya makada 58 kuchukua fomu za kuwania ubunge kupitia CCM kwenye majimbo nane ya Mkoa wa Iringa, mpaka jana ,Julai 19.

Takwimu zilizopatika zinaonesha kuwa, majimbo yanayoongoza kwa kuwa na wagombea wengi ni Kalenga-Iringa vijijini makada 13, Iringa Mjini makada 12, Njombe Kaskazini 11, Njombe Magharibi tisa, Makete wanne, Kilolo watatu, Mufindi Kaskazini watatu na Njombe Kusini wawili.

Ushindani mkali unaonesha kuwa katika jimbo la Manispaa ya Iringa lililokuwa linashikiliwa na Monica Mbega na Njombe Kaskazini ambalo lilikuwa likishikiliwa na Jackso Makweta.

Mpaka jana jumatatu julai 19, Mwenyekiti wa CCm Mkoa wa Iringa,Deo Sanga, maaru kama Jah People pia alichukua fomu kupambana na mbunge huyo wa siku nyingi,Jackson Makweta.

Katibu wa CCM wilaya ya Njombe Osea Mpagike aliwataja wengine wanaowania jimbo la Njombe Kaskazini kuwa ni Musa Mgata, Dickson Mtikwa, Jackson Makweta, Alatanga Nyagawa, Martin Chodota, Joachim Kinyunyu, Lena Hongeli, Laula Malecela, Onesmo Kinine na Julius Ngeme.

Kwa upande wa Jimbo la Iringa mjini, wanaoinyemelea ni Frederick Mwakalebela, Ado Mwasongwe, Fadhili Ngajilo, Yahya Msigwa, Jesca Msambatavangu, Thomas Kimata, Dkt. Kalinga, Monica Mbega, John Kiteve, Ben Mpete, Cherestino Mofuga na Zuberi Mwachura.

Kaimu Katibu CCM wilaya ya Iringa ambaye ni Katibu wa vijana, Pius Seleman alisema waliochukua fomu katika jimbo la Isimani ni Festo Kiswaga na Yahya Mtete wakati William Lukuvi anatarajia kuchukua siku ya mwisho na kuirudisha.

Alisema Jimbo la Kalenga ni Bruceson Kibasa, Abbas Kandoro, Anjero Mbunda, Stanslaus Mhongole, Anejlus Kisiga, Dkt. William Mgimwa, Victor Masangula, Hafsa Mtasiwa, Edward Mtakimwa, Richard Mfalingundi, Gabriel Kalinga, George Mlawa, Anset Sambala na Leonard Mwalu wakati kwa upande wa Jimbo la kilolo ni Profesa Peter Msola, Stephen Mwaduma na Venance Mwamoto ambao wote wamewahi kushika nafasi hiyo kwa vipindi tofauti.

Jimbo la Mufindi Kaskazini ni Jeseph Mungai, Mahamud Mgimwa, na Alamu Mwawaya na kwa upande wa Jimbo la Makete ni Benedict Mahenge, Amalaki Ngajilo, Zilumba Sanga, Anna Luvanda na Norman Sigalla.Jimbo la Njombe Kusini ni Anna Makinda na Demist Msemwa, jimbo la Njombe Magharibi ni Yono Kevela, Isaya Manjele, Japhet Mlagala, Graham Ngela, Thomas Nyimbo, Solomoni Nongono, June Ngole, Geison Lenge na Yahya Chaula.

Mwisho wa kurudisha fomu za kuwania kuteuliwa nafasi hiyo ni kesho jumatano, julai 21 ambapo itajulikana na ni makada wangapi wameingia katika kinyang’anyiro hicho.

No comments:

Post a Comment