McEddy Elroy

Saturday, October 1, 2011

Kadri unavyoelekea Ihefu,mto Ruaha Mkuu unapata uhai

UMWAGILIAJI SAWA,UMEME NAO JE?????????????

Ukichunguza kwa makini,utabaini kwamba uchache wa mvua katika misimu miwili iliyopita siyo chanzo pekee cha kukauka kwa mto Ruaha Mkuu na hatimaye kukauka kwa bwawa la Mtera na mabwawa mengine kama Kidatu na Kihansi.

Kilimo cha umwagiliaji kinachopigiwa upatu mkubwa sana na tamko la Kilimo kwanza, ambacho hufanyika katika maeneo mbalimbali hususani maeneo ya Kapunga huko Mbarali, karibu kabisa na chanzo cha mto Ruaha Mkuu huko katika eneo oevu la Ihefu,kimekuwa ni chanzo kikubwa cha kukauka mto huo.

Kingine ni siasa chafu za baadhi ya wanasiasa wanajali zaidi maslahi yao na kuacha maslahi ya Taifa.Mathalani, Serikali ilikwishatangaza hadi kwenye gazeti la Serikali kwamba eneo flani liihifadhiwe na watu wote waliokuwepo waondoke ili uoto wa asili urejee na hivyo kutiririsha maji mwaka mzima lakini anaibuka mtu mmoja tu tena anayetaka ubunge na kuanza kuwalaghai wananchi kwamba Serikali ilifanya makosa na hivyo wakimchagua yeye atahakikisha wanarejea kwenye eneo hilo,ni nini hiyo kama siyo siasa chafu isiyozingatia maslahi ya Taifa na kwa hakika siasa kama hiyo inaweza kulitumbukiza Taifa katika vurugu na wananchi wake.

Ukiungalia mto Ruaha Mkuu kwa sasa, hauna matumaini kabisa kwa Taifa hili kwa upande wa umeme.Lakini mto huo unaonesha matumaini kidogo kadri unavyoelekea kwenye chanzo chake huko Ihefu.Kumbuka Ihefu ni matokeo ya maamuzi magumu yaliyofanywa na Serikali takribani miaka mitano iliyopita kwa kuwaondoa wafugaji waliokuwa wamevamia eneo hilo.

Kwenye hifadhi ya Ruaha,mto huo umebaki kuwa na hali ya madimbwi madogo madogo ambayo kwa sasa ndiyo uanaokoa wanyama waliomo humo lakini ukiufuatilia hadi Ihefu, utagundua kuwa,kadri unavyoelekea Ihefu, ndivyo unavyokuwa na uhai kidogo kama picha hapo juu, inavyoonesha.

Friday, September 30, 2011

NYATI WAKINYWA MAJI MTO RUAHA MKUBWA,KAMA WALIVYONASWA KUTOKEA ANGANI

MTO RUAHA MKUBWA WABAKI MADIMBWI,HAKUNA MATUMAINI YA UMEME

Maji yanaendelea kuwa bidhaa nadra sana nchini.Hali ya Mto Ruaha Mkubwa (The Great Ruaha) ambao unategemewa sana na mabwawa yanayotumiwa na Shirika la Ugavi wa umeme nchini Tanzania (Tanesco) ya Mtera,Kidatu na Kihansi kuzalisha nishati hiyo, uko katika hali mbaya sana na kwa hakika hakuna matumaini kabisa kama mvua zitachelewa kunyesha.
Blog huu imetenbelea hifadhi ya ruaha wiki iliyopita na kufanikiwa kupata picha mbalimbali za mto huo hapo September 28,mwaka huu, zinaonesha namna hali ilivyo mbaya hali inayotishia ustawi wa hifadhi ya ruaha.
Historia ya hifadhi ya Ruaha haiwezi kutenganishwa na Mto Ruaha Mkuu au Mto Ruaha Mkubwa hivyo bila uwepo wa mto Ruaha Mkubwa, mimea na uoto mwingine wa asili utatoweka vivyo hivyo kwa wanyama ambao ni rasilimali kubwa ya Taifa la Tanzania.
Kwa sasa Hifadhi ya Taifa ya Ruaha ni kubwa kuliko hifadhi yoyote nchini ikiwa na meta za mraba 20,000 (Elfu ishirini).Ruaha pia ni ya pili kwa ukubwa barani Afrika ikifuata kwa karibu kwa hifadhi ya Salonga iliyoko nchini Jamhuri ya Kidemocrasia ya watu wa Congo.
Tutaendelea kukuletea habari hii kwa kina zaidi. Endelea kuwa nasi.

MTO RUAHA MKUBWA WABAKI MADIMBWI,HAKUNA MATUMAINI YA UMEME

Tuesday, June 7, 2011

MWAKILISHI MSAIDIZI WA THE GUARDIAN IRINGA AFARIKI DUNIA

MFANYAKAZI wa Kampuni ya The Guardian Ltd Mkoani Iringa, Isdory Fungo (41) amefariki dunia.
Fungo alifariki dunia alfajiri ya Juni 07,mwaka huu katika hospitali ya Wilaya ya Makete alikokimbizwa baada ya hali yake kubadilika ghafla.
Taarifa iliyotolewa na Mwakilishi wa Kampuni ya The Guardian Mkoa wa Iringa, Kishede Msuya imesema awali, Fungo alikuwa anaugua malaria na miguu ambapo alipata matibabu Mjini Iringa kabla ya kwenda hospiatli ya Misheni ya Ikonda wilayani Makete kwa matibabu zaidi ambako alilazwa kwa wiki moja na kurejea kwa kaka yake Mjini Makete.
Hata hivyo,akiwa nyumbani kwa kaka yake usiku wa kuamkia jana hali yake ilibadilika ghafla ambapo alikimbizwa katika hospitali ya wilaya ya Makete lakini alifariki dunia muda mfupi baadaye.
Kampuni ya The Guardian inaungana na wafiwa katika msiba huo, ambao marehemu Isdory atazikwa nyumbani kwao Makete.
Kabla ya kuajiriwa na kampuni ya The Guardian mwaka 2008 alikuwa wakala wa magazeti ya kampuni mbalimbali katika kituo cha Makambako wilayani Njombe,kazi ambayo aliifanya kwa zaidi ya miaka 10.
Hadi kifo chake hapo jana,Fungo alikuwa Mwakilishi Msaidizi wa Mkoa wa Iringa wa kampuni ya The Guardian Ltd. Marehemu ameacha mjane na mtoto mmoja.

NIMEREJEA NDUGU ZANGU NAOMBA MNIUNGE MKONO

Wapenzi wasomaji wangu wa blog hii.Naahidi kwamba kwa sasa nimerejea kwa kishindo kukuketea mambo uliyoyakosa kwa muda mrefu.Kwa takribani miezi miwili na nusu nimekuwa sipo sana hewani baada ya computer yangu kuibwa na watu ambao mpaka leo hawajulikani.
Nimejikongoja na nimenunua Computer nyingine na sasa nimerejea tena katika ulingo huu wa upashanaji na uelimishaji jamii yetu.
Twende pamoja.Tanzania yetu sote.