McEddy Elroy

Thursday, August 19, 2010

KIPYENGA CHAPULIZWA RASMI MAJIMBONI

Agosti 19:VIGOGO wawili wa CCM wa Mkoani Iringa waliotimkia Chadema,Alatanga Nyagawa na Thomas Nyimbo wamerejesha fomu za Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) za kuwania ubunge kwa tikiti ya chama hicho katika Majimbo ya Njombe Kaskazini na Njombe Magharibi.

Tofauti na Majimbo mengine, kama watapitishwa na NEC, watakaopambana Jimbo la Njombe kaskazini ni Deo Sanga, ambaye ni Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Iringa na Alatanga Nyagawa wa Chadema.

Aidha,Jimbo la Njombe Magharibi watakaopambana pia ni wawili tu ambao ni Thomas Nyimbo wa Chadema ambaye amewahi kuwa Mbunge wa Jimbo hilo kwa tikiti ya CCM kwa kipindi cha miaka kumi ambaye atapambana Gelson Lwengwe wa CCM.

Kwa upande wa kilolo, Prof.Peter Msolla ambaye wakati akirejesha fomu mamia ya watu waliandama naye, atapambana na Cray Mwituka wa Chadema na mwana mama Mwaka Mgimwa wa chama cha Chausta.

“Nawashukuru wananchi kwa kuonesha imani kwangu na nitajihadi kuwahudumia vyema ili niwe mbunge wao wa kudumu kama wanavyoomba,” alisema Msolla ambaye alikuwa akijibu maombi ya wananchi waliokuwa wakiimba kutaka awe mbunge wao wa kudumu.

Wengine waliorejesha fomu hadi jana saa 9:00 alasiri ni kama ifuatavyo:

Mufindi Kusini.
Menrad Kingola (CCM).

Mufindi Kasikazini.
Mahamud Mgimwa (CCM) na Lawrance Mwabusi (NCCR-Mageuzi).

Jimbo la Kalenga.
Dr.William Mgimwa (CCM),Rehema Makoga (Chadema), Makuke Mginja (Jahazi Asilia) na John Lumuliko (TLP).

Jimbo la Isimani.
Benny Kapwani (Chadema), William Lukuvi (CCM) na Mussa Fufumbe (CUF).

Jimbo la Iringa Mjini.
Monica Mbega (CCM) na Mchungaji Peter Msigwa (Chadema).

Mwisho.

No comments:

Post a Comment